Ili kuhakikisha huduma bora zaidi, tunatumia faili ndogo zinazoitwa kuki. Wakati wa kutumia wavuti yetu, faili za kuki zinapakuliwa kwenye kifaa chako. Unaweza kubadilisha mipangilio ya kivinjari chako wakati wowote. Kwa kuongezea, utumiaji wako wa wavuti yetu ni sawa na idhini yako kwa usindikaji wa data yako ya kibinafsi inayotolewa na njia za elektroniki.
Kwenda Nyuma

Maonesho ya Elimu ya Umoja wa Ulaya jijini Dar es Salaam

17.05.2022

Ubalozi wa Poland ulishiriki kikamilifu katika Maonesho ya Elimu ya Umoja wa Ulaya ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Ulaya nchini Tanzania yaliyoandaliwa na wawakilishi wa Umoja wa Ulaya.

EU_Edu_Fair UDSM_4

Siku ya Jumamosi tarehe Mei 14, 2022, katika kampasi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Yalifanyika maonyesho ya Elimu ya Umoja wa Ulaya mwaka 2022. Kusoma nchini Poland ni maarufu sana miongoni mwa vijana wa Kitanzania ambao wanaweza kushiriki katika Mpango wa Masomo ya Banach. Stendi yetu ilitembelewa na zaidi ya watu 500! Ubalozi uliwakilishwa na balozi Piotr Kruze na mkuu wa utawala na fedha, Edgar Klusa. Inafaa kukumbukwa kuwa maonyesho hayo yalihudhuriwa na mwakilishi wa Chuo Kikuu cha Maria Curie-Sklodowska huko Lublin (UMCS), Dkt. Konrad Czernichowski, ambaye hotuba yake kwa Kiswahili ilisababisha shangwe kubwa miongoni mwa hadhira.

Picha (5)

{"register":{"columns":[]}}