Ili kuhakikisha huduma bora zaidi, tunatumia faili ndogo zinazoitwa kuki. Wakati wa kutumia wavuti yetu, faili za kuki zinapakuliwa kwenye kifaa chako. Unaweza kubadilisha mipangilio ya kivinjari chako wakati wowote. Kwa kuongezea, utumiaji wako wa wavuti yetu ni sawa na idhini yako kwa usindikaji wa data yako ya kibinafsi inayotolewa na njia za elektroniki.
Kwenda Nyuma

Shukrani kwa Mfuko wa Msaada wa Poland, Watoto kutoka katika Milima ya Usambara tayari wanafaidika na chumba cha pili cha ziada cha mtaala wa kawaida

09.12.2021

Mwaka huu, Shukrani kwa ushiriki wa mshirika wa ndani -A.D. Views Management Ltd. na fedha zilizochangwa kama sehemu ya ushirikiano wa maendeleo wa Poland na Ubalozi wa Jamhuri ya Poland jijini Dar es salaam, tayari takribani wasichana na wavulana 300 kutoka wilaya ya Lushoto katika milima ya Usambara kaskazini mwa Tanzania wanahudhuria vyumba vilivyopangwa maalum vinavyotoa sio tu mahali salama pa kucheza, lakini juu ya yote kujifunza.

Świetlica_w_Usambara 2021_7

Kama sehemu ya mradi wa mwaka huu wa "Sisterhood Land 2”, ikiwa ni ufuatiliaji wa mradi wa mwaka jana, vyumba zaidi ambapo watoto wanaweza kusoma kitabu, kufanya kazi zao za nyumbani za hesabu au kucheza tu na kupumzika vimekarabatiwa na kuwekwa fenicha. Maktaba ya kituo hicho imewekwa vitabu vya kiada ambavyo watoto wanaweza kutumia papo hapo au wanaweza kuazima ili kutumia nyumbani.

Tangu kuzinduliwa kwake, mradi huu umekuwa maarufu sana miongoni mwa jamii ya eneo hilo na umevutia watoto zaidi na zaidi wanaotafuta hali bora ya kujifunza na kukuza ujuzi wao, vipaji, na pia uwezo wao wa kuingiliana na wenzao. Katika maisha ya kila siku, wavulana na wasichana katika milima ya Usambara wanakabiliwa na vikwazo vingi katika njia yao ya kupata elimu bora: hawana nafasi ya kutulia kuweza kuzingatia masomo yao, wanaelemewa na idadi kubwa ya kazi za nyumbani, wakati wazazi wao hawajihusishi na elimu yao. Kwa hivyo, kufunguliwa kwa kituo cha elimu kwa msaada wa fedha za Poland ni fursa ya kipekee ya elimu bora kwa wanafunzi hawa.

Hapo awali, mradi ulilenga tu kwa wasichana, ambao wanaunda kundi la kijamii lisilo na kipaumbele  nchini Tanzania katika masuala ya kielimu na maendeleo ya kiakili na kihisia, na lengo lake lilikuwa kujenga uwezo wa sehemu ya mwanamke katika jamii katika wilaya ya Lushoto, kuwapa maandalizi bora ya maisha ya kila siku na kazi. Hata hivyo, mafanikio ya mradi huo mwaka jana yalidhihirisha kupendezwa na mradi huo kwa upande wa wavulana, ndiyo maana mwaka huu, mbali na vyumba vya wasichana, chumba kipya cha wavulana pia kimefunguliwa katika shule ya msingi iliyopo Mtae.

 

 

 

Picha (8)

{"register":{"columns":[]}}